Jumanne, 3 Septemba 2013

KWA UMOJA HUU, LIGI YA MKOA MBEYA AIRPORT RANGERS F.C MOTO WA KUOTEA MBALI

USHINDI JADI YETU
Vijana wa Airport rangers wakiwa katika mazoezi  ya viungo katika uwanja wa uhasibu mjini mbeya ikiwa ni mfululizo wa mazoezi kama moja ya  maandalizi ya ligi ya mkoa (mbeya)  2013.  ligi hiyo ikiwa inatarajiwa kuanza mapema mwezi wa kumi na kurindima katika viwanja mbalimbali katika mkoa huu wa mbeya.
Vijana wanakila sababu za kuvuka kwenda katika ligi ngazi ya taifa kwani timu imesheheni wachezaji wenye uwezo wa hali ya juu na nidham ya pekee , kwani hufanya mazoezi kwa pamoja,vijana hawa wamekua wakionyesha mabadiliko chanya kimpira kadiri siku zinavyo zidi kwenda Mbele, huwai kufika mzaoezini mapema kama kocha wao awaelekezavyo nani vijana wenye usikivu wa namna yake pale wanapo pewa maelekezo na waalim wao.
Mazoezi hufanyika kila siku kuanzia jumatatu mpaka jumamosi katika uwanja wa uhasibu kuanzia saa 10 kamili mpaka saa12 kamili jioni, wape support vijana hawa hata kwa kufika uwanjani kutizama kile wakifanyacho kama wachezaji mda huo wa join katika siku za juma.
Bwana Yusuph Mlekwa na kijana Boaz  Mwakibete  ndio waalim wakuu waliopewa dhamana ya kuifundisha timu hii  kwa kipindi hiki kigumu cha maandalizi mpaka hapo baadae.







0 maoni:

Chapisha Maoni